Published 2024-05-16 13:54:16 by JKCI
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika kuadhimisha siku ya shinikizo la damu duniani inafanya upimaji wa magonjwa ya shinikizo la damu, sukari na moyo kwa wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam na mikoa ya jirani.Upimaji huo ujulikanao kwa jina la Mhe. Samia Suluhu Hassan Outreach Services umeanza kufanyika leo katika Hosptitali ya JKCI Dar Group na utamalizika kesho tarehe 17 Mei 2024 kwa kutoa huduma bila gharama kwa wananchi wote watakaojitokeza kufanyiwa uchunguzi wa magonjwa hayo.Akizungumza na waandishi wa habari daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Hospitali ya JKCI Dar Group Baraka Ndelwa alisema upimaji huo unafanyika ili kuwapa nafasi wananchi kuufahamu vizuri ugonjwa wa shinikizo la juu la damu na namna ambavyo wanaweza kujikinga na ugonjwa huo.Dkt. Baraka alisema upimaji huo unatolewa bila gharama ili kuwafikia wananchi wenye kipato cha chini kufanyiwa uchunguzi, kupatiwa matibabu na wale watakaohitaji dawa kupatiwa bila gharama.“Tunazishukuru kampuni za dawa za binadamu zilizoshirikiana nasi katika kuadhimisha siku ya shinikizo la damu duniani kwa kuwaletea wagonjwa wetu dawa bila gharama”, alisema Dkt. BarakaKwa upande wake mwananchi aliyepatiwa huduma katika kambi hiyo Paulina Lwegeta alisema hakujua kama ana tatizo la shinikizo la juu la damu lakini kwasababu ndugu yake ana tatizo hilo na amelazwa katika hospitali JKCI Dar Group akaamua naye atumie nafasi aliyopata kuchunguza afya yake.“Kupitia matokeo niliyoyapata hapa naona watu wengi tutakuwa tunaumwa ugonjwa wa shinikizo la juu la damu lakini hatujui, natoa wito kwa wananchi wenzangu kuwa na tabia ya kufanya vipimo mara kwa mara”, alisema PaulinaPaulina alisema amekuwa akiumwa kichwa kwa muda mrefu lakini hakujua kama ana tatizo la shinikizo la juu la damu hadi leo alipofanyiwa uchunguzi na kugundulika kuwa na tatizo hilo ambapo amepatiwa dawa.Omary Seif mkazi wa Temeke alisema amekuwa akisumbuliwa na tatizo la shinikizo la juu la damu kwa muda mrefu na kupatiwa matibabu katika hospitali tofauti bila ya mafanikio.“Nimekuwa nikitibiwa tatizo la shinikizo la damu tangu mwaka 2022 katika hospitali tofauti lakini chaajabu hakuna siku presha yangu imeshuka na kukaa sawa, siku zote ipo juu hadi imeniletea matatizo ya macho kwani sasa hivi sioni vizuri”, alisema OmaryOmary alisema baada yakuona matangazo ya upimaji unaofanyika JKCI Dar Group alichukua hatua yakufika katika upimaji huo ambapo amepata huduma na kushauriwa vizuri kuhusu dawa alizokuwa anatumia hapo awali.Naye meneja kutoka kampuni ya dawa za binadamu ya Hetero Lab Ivan Edmund alisema kampuni mbalimbali za dawa za binadamu kwapamoja zimeungana kushirikiana na JKCI kuwapatia wananchi watakaokuta na matatizo ya shinikizo la damu, sukari na magonjwa ya moyo dawa bila gharama.Ivan alisema kulingana na hali za wananchi wengi kampuni yake na nyingine zilizojitokeza hazikuona shida kuadhimisha siku ya shinikizo la damu duniani na wananchi watakaojitokeza kupima katika kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inayofanyika JKCI Dar Group.“Tunaishauri jamii iache matumizi ya dawa bila ya kumuona daktari ni vizuri kabla ya kutumia dawa ukamuona daktari akakufanyia uchunguzi na kukuandikia dawa sahihi kwani dawa ni tiba na wakati mwingine dawa inaweza kuwa sumu isipotumika vizuri”, alisema Ivan
Published 2024-05-16 10:40:26 by JKCI
Zaidi ya asilimia 60 ya watu wenye shinikizo la juu la damu hapa nchini hawajitambui kama wana tatizo hilo kwani tafiti zinaonesha kati ya watu kumi watu watatu ndio wanatambua kuwa na tatizo hilo.Hayo yamesemwa na Kaimu Mkuu wa Hospitali ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group Dkt. Tulizo Shemu leo jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu siku ya shinikizo la damu duniani inayoadhimishwa kila ifikapo Mei 17.Dkt. Shemu alisema Ugonjwa wa shinikizo la juu la damu unatokana na madhara ya kiwango cha presha kuwa kikubwa katika mwili wa binadamu hivyo kusababisha shinikizo la damu kuwa juu.“Ugonjwa wa shinikizo la juu la damu hauna dalili maalumu lakini zipo dalili chache zinazoweza kujitokeza endapo mtu atapata ugonjwa huu zikiwemo dalili ya kuumwa kichwa mara kwa mara, macho kutoona vizuri, moyo kwenda haraka, pamoja na kubanwa na kifua”, alisema Dkt. ShemuDkt. Shemu alisema Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete inaenda kuadhimisha siku hiyo kwa kufanya upimaji bila gharama tarehe 16 na 17 May 2024 katika Hospitali ya JKCI Dar Group lengo likiwa kuleta uelewa na ufahamu katika jamii kuhusu tatizo la shinikizo la juu la damu.“Kauli mbiu ya mwaka huu inatutaka kuzifahamu tarakimu za shinikizo la damu kwa kupima presha kwa usahihi na endapo utakutwa na ugonjwa huu hakikisha unapata matibabu na kudhibiti ugonjwa ili usiweze kukuletea madhara mengine yatokanayo na tatizo la presha”, alisema Dkt. ShemuDkt. Shemu alisema kwa takwimu zilizofanyika kwa wagonjwa wanaotibiwa JKCI mwaka 2023 kati ya wagonjwa 125,927 waliopatiwa matibabu asilimia 42 walikuwa na shinikizo la juu la damu.“Madhara ya ugojwa huu ni pamoja na kupata kiharusi, kusababisha figo kushindwa kufanya kazi, kupata magonjwa ya mshtuko wa moyo, tatizo la moyo kushindwa kufanya kazi, kuvimba miguu, kupata ganzi sehemu za mwili, kupumua kwa shida, kukosa nguvu pamoja na shida za uzazi”, alisema Dkt. ShemuNaye daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sulende Kubhoja alisema tatizo la shinikizo la juu la damu huwapata pia watoto na tatizo hilo hutokana na matatizo mengine ambayo mtoto anakuwa nayo.Dkt. Kubhoja alisema tunapoenda kuadhimisha siku ya shinikizo la damu tusiwasahau watoto kuwashirikisha upande wa kufanyiwa uchunguzi na hata eneo la kupata elimu kuhusu ugonjwa huo ili pale wanapoweza kujikinga wajikinge.“Mara nyingi ukimkuta mtoto ana shinikizo la juu au la chini la damu hutokea kama mtoto ana matatizo ya figo, au matatizo mengine katika viungo vinavyowasiliana mwilini”, alisema Dkt. KubhojaDkt. Kubhoja alisema kuna watoto wamekuwa wakipata tatizo la shinikizo la juu la damu kutokana na magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa pamoja na matatizo ya mishipa ya damu kuwa na hitilafu.“Sisi tunapopata mtoto ana tatizo la shinikizo la juu la damu tunamfanyia uchunguzi kwa kuangalia kila kiungo cha mwili wa mtoto ili tuweze kutambau sehemu yenye matatizo na kuweza kuitibu” alisema Dkt. Kubhoja
Published 2024-05-06 13:18:22 by JKCI
Kwa mara ya kwanza upasuaji wa kurekebisha valvu za moyo kwa watu wazima umefanyika kwa mgonjwa ambaye valvu yake ya moyo ya upande wa kushoto ilikuwa ikivujisha damu (severe mitral regurgitation).Upasuaji huo umefanywa hivi karibuni na madaktari bingwa wa upasuajia wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na mwenzao kutoka Serikali ya Watu wa China.Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Williams Ramadhan alisema upasuaji wa kurekebisha valvu za moyo umekuwa ukifanyika kwa watoto wenye shida za valvu lakini kwa watu wazima mgonjwa huyo amekuwa wa kwanza kurekebishiwa valvu yake kwani wagonjwa wengine wamekuwa wakiwekewa valvu za bandia.“Upasuaji wa kurekebisha valvu za moyo mara nyingi umekuwa ukifanyika upande wa watoto kwa mafanikio makubwa lakini haufanywi upande wa upasuaji wa moyo kwa watu wazima kwani matibabu hayo yanahitaji utaalamu wa hali ya juu lakini pia mafanikio huongezeka pale daktari husika anapokuwa amefanya idadi kubwa ya upasuaji huo”.“Ukimfanyia mgonjwa upasuaji wa kurekebisha valvu za moyo na usifanikiwe utahitaji kurudia kufanya upasuaji tena mara ya pili hivyo kumuongezea mgonjwa muda ya kukaa kwenye mashine na kumpa wasiwasi”, alisema Dkt. RamadhaniDkt. Ramadhani alisema mara nyingi kwasababu wataalamu wa JKCI wa upasuaji mkubwa wa moyo kwa watu wazima bado hawajatoa huduma hiyo kwa wagonjwa wengi wamekuwa wakifanya upasuaji wa kubadilisha valvu za moyo na si kurekebisha valvu za moyo.“Tunaushukuru uongozi wa Taasisi kutuletea mtaalamu kutoka China anayefanya upasuaji wa kurekebisha valvu za moyo kwa wagonjwa watu wazima ambao valvu zao zinaweza kurekebishwa na kupona ambaye kwa kipindi cha miaka miwili tutakachokuwa naye hapa atatuongezea ujuzi zaidi”, alisema Dkt. Ramadhan.Kwa upande wake Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kutoka Serikali ya watu wa China Liu YiMin alisema upasuaji huo kwake umekuwa wa kwanza kuufanya tangu afike katika Taasisi hiyo na kuweza kubadilishana ujuzi na wataalamu wenzake wa JKCI.Dkt. Liu alisema matibabu ya kurekebisha valvu za moyo humsaidia mgonjwa kuishi bila ya kutumia dawa za kuzui damu kuganda (Anticoagulants) katika maisha yake tofauti na mgonjwa ambaye valvu yake ya moyo imebadilishwa na kuwekewa ya bandia hulazimika kutumia dawa maisha yake yote ili kuzuia damu isigande“Mgonjwa aliyebadilishiwa valvu za moyo uhitaji kutumia dawa ya warfarin hivyo kumlazimu kupima damu yake mara kwa mara kuangalia kama inaganda tofauti na mgonjwa huyu ambaye tumemrekebishia valvu yake hivyo haitaji kutumia warfarin”, alisema Dkt. Liu YiMin.Dkt. Liu alisema wagonjwa waliobadilishiwa valvu za moyo wakati mwingine hupata tatizo la kuvuja damu hivyo kuwa katika hatari na kuhitaji kuonana na wataalamu wa afya mara kwa mara.“Upasuaji huu wa kurekebisha valvu za moyo hasa kwa wanawake huwapa wagonjwa nafasi ya kutengeneza familia kwani mwanamke anapokuwa katika kipindi cha ujauzito hatakiwi kutumia dawa mbalimbali ikiwemo dawa ya warfarin”, alisema Dkt. Liu.Naye mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa kurekebisha valvu ya kushoto ya moyo kutoka mkoani Mtwara Ismail Stambuli alisema amekuwa akisumbuliwa na tatizo la moyo na shinikizo la damu kwa muda mrefu tatizo ambalo hakutegemea kama ingefikia kufanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo.Ismail alisema tatizo la moyo amekuwa nalo tangu utotoni na kuonyesha dalili moja ya kutokwa na jasho kwa wingi lakini kwasababu hakujua kama kutokwa na jasho kwa wingi ni dalili ya magonjwa ya moyo hakuwahi kufuatilia matibabu hadi sasa alipokuwa akisumbuliwa na typhoid mara kwa mara hivyo kulazimika kufanyiwa uchunguzi zaidi na kugundulika kuwa na tatizo la valvu ya kushoto ya moyo.“Nawashukuru sana wataalamu wa JKCI kwa kugundua tatizo langu na kulitibu kwasababu sikuwa na dalili na ilikuwa hatari kwangu maana ningeendelea na maisha kama kawaida kumbe nina tatizo kubwa katika moyo wangu”, alisema Ismail.
Published 2024-05-06 13:10:30 by JKCI
Wananchi wametakiwa kuunga mkono jitihada za Serikali kushiriki katika mazoezi ya pamoja kupambana na magonjwa yasiyoambukiza.Rai hiyo imetolewa leo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakati akizindua mazoezi ya pamoja yaliyofanyika katika viwanja vya Coco beach jijini Dar es Salaam.Mhe. Kassim Majaliwa alisema wananchi wanatakiwa kutenga siku angalau moja kila wiki kufanya mazoezi ili kupunguza changamoto za magonjwa yasiyoambukiza.“Mazoezi haya ya pamoja ambayo nimeyazindua rasmi leo hapa Dar es Salaam yatafanyika nchi nzima ikiwa ni mkakati wa kupunguza magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo magonjwa ya shinikizo la damu, sukari na msongo wa mawazo”, alisema Mhe. Kassim MajaliwaMhe. Kassim Majaliwa alisema kuanzia leo barabara inayotoka Coco beach kuelekea daraja la tanzanite hadi makutano ya barabara ya hospitali ya Aga khan kuelekea Taasisi ya Ocean Road itakuwa ikifunga kila siku ya jumamosi kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa tatu asubuhi kuwapa nafasi watu wa Dar es Salaam kufanya mazoezi bila ya kuwa na msongamano wa magari.Kwa upande wake Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu alisema kumekuwa na ongezeko kubwa la magonjwa yasiyoambukiza hivyo kama wizara ya afya inatekeleza wajibu wake mkuu wa kuwakinga watanzania na magonjwa hayo. “Mwaka 2016 hadi 2019 wakati nawasilisha bajeti ya wizara ya afya kati ya magonjwa kumi yanayowasumbua watanzania hakukuwa na ugonjwa hata mmoja wa magonjwa yasiyoambukiza lakini hadi kufikia mwaka 2021 magonjwa hayo yameongezeka kwa kasi hivyo kuingizwa katika bajeti ya wizara ya afya”, alisema Mhe. UmmyMhe. Ummy alisema mazoezi yanasaidia kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza ususani magonjwa ya shinikizo la juu la damu na kisukari kwa zaidi ya asilimia hamsini.“Wizara ya afya pamoja na kuweka nguvu kwenye kujenga hospitali na kununua dawa tutaweka nguvu kwaajili ya kuwakinga watanzania wasipate magonjwa yasiyoambukiza kwa kuhamasisha mazoezi na mtindo bora wa maisha”, alisema Mhe. UmmyAkizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge Kaimu Mkuu wa Hospitali ya JKCI Dar Group Dkt. Tulizo Shemu alisema kufanya mazoezi kunamsaidia mtu kupunguza kiwango kikubwa cha rehemu katika mwili.“Kila dadika kumekuwa kukitokea vifo kutokana na matatizo ya magonjwa yasiyoambukiza hivyo kwakufanya mazoezi kunapunguza athari za kuweza kupoteza maisha kutokana na magonjwa hayo”, alisema Dkt. ShemuDkt. Shemu alisema tafiti zilizofanyika hivi karibuni zinaonyesha kwenye miji mikubwa kama Dar es Salaam watu wazima watano hadi sita kati ya watu 10 wana shinikizo la juu la damu ambapo wagonjwa wengi wanapata shinikizo la damu kutokana na mtindo wa maisha na kuwa na rehemu nyingi.“Tukiwa na taratibu za kufanya mazoezi mara kwa mara tutakuwa tumeweza kupunguza kiwango kikubwa cha magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo magonjwa ya moyo na kuongeza nguvu kazi katika nchi yetu”, alisema Dkt. Shemu
Published 2024-05-06 13:06:10 by JKCI
Wataalamu kutoka Wizara ya Afya nchini Sierra Leone wametembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kujifunza namna ambavyo taasisi hiyo imepiga hatua kubwa katika matibabu ya moyo barani Afrika.Wakiwa katika Taasisi hiyo wataalamu hao walijifunza namna ambavyo matibabu ya moyo yalivyoimarika nchini kutokana na mambo matatu ikiwemo utayari wa Serikali kuwekeza kwenye matatibu ya moyo.Mbinu zingine ni Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kusambaza dawa kwenye taasisi hiyo na mfumo wa manunuzi na uendeshaji wa huduma za kifamasia unavyofanyika, ushirikiano wa watendaji ndani ya taasisi pamoja na matumizi ya mifumo ya Tehama kwenye matibabu.Uwekezaji kwenye mifumo ya Tehama katika matibabu na utayari wa Serikali kuwekeza ni mambo aliyoyatajwa kuwa ni muhimu wakayafanyie kazi wanapokwenda kuanzisha taasisi ya moyo.Mganga Mkuu wa Serikali ya Sierra Leone Dkt. Sarfie Kenneth ambaye aliongoza timu ya wataalamu hao 11 kuja nchini, alisema Tanzania kwenye eneo la matibabu imepiga hatua ndio maana wamekuja kujifunza.Dkt. Keneth alisema ni muhimu kwa nchi za Afrika kushirikiana kufanya kazi kwa pamoja husasan kwenye uimarishaji wa sekta ya afya."Tiba nyingi za kibingwa zinafanyika nje ya mataifa ya Afrika hivyo kuwa na taasisi kama JKCI ni hatua kubwa ambapo pia tunapaswa kuweka ushirikiano, lakini tumeona utayari wa Serikali ni uti wa mgongo kwa kila kitu kufanyika", alisema Dkt. Keneth.Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema matunda ya ziara hiyo ni kuvutia utalii tiba."Wenzetu wamekuja kujifunza namna ambavyo tumepiga hatua na tumewaeleza namna Serikali ilivyoamua kuwekeza kwenye matibabu kwa kuajiri wataalamu na kununua vifaa, pia wamejifunza kuanza kuleta wagonjwa hapa nchini kutokana na ambavyo wameona huduma zinavyotolewa na hii ni sehemu ya utalii tiba”, alisema Dkt. Kisenge.Naye Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa JKCI Dkt. Delilah Kimambo alisema matibabu ya moyo si ya daktari peke yake bali ni ushirikiano wa wataalamu mbalimbali hivyo aliwaeleza wataalamu kutoka Sierra Leone ushirikiano wa wataalamu kwenye taasisi hiyo ndiyo kiungo muhimu kwa usalama wa wagonjwa.Ziara hiyo ya wataalamu kutoka Wizara ya Afya nchini Sierra Leone ilikuwa ni ya kujifunza namna JKCI ilivyopiga hatua na mbinu walizotumia kwa lengo la kwenda kutumia mbinu hizo kuanzisha taasisi kama hiyo nchini humo.
Published 2024-04-24 07:10:50 by JKCI
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imeanza kutoa huduma ya kuwafuata wagonjwa manyumbani mwao na kuwapa tiba wanayostahili.Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu huduma hiyo.Dkt. Kisenge ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo alisema huduma hiyo itasaidia kupunguza vifo vya ghafla vya wagonjwa pamoja na kuokoa muda wa kuwapeleka hospitali. Mkurugenzi huyo Mtendaji alisema huduma hiyo itakuwa ni maalumu kwa wagonjwa ambao walilazwa hospitali na wameruhusiwa kurudi nyumbani lakini pia wanahitaji kupata huduma ya uangalizi maalumu kwani wagonjwa hao shinikizo lao la damu linaweza kushuka au kuwa juu sana na kuwasababishia kifo cha ghafla.“Hii ni huduma mpya ya teknelojia ya hali ya juu ambapo chini ya godoro la mgonjwa kitawekwa kifaa maalumu kinachojulikana kwa jina la DOZEE ambacho kinamtetemo na kuweza kusoma shinikizo la damu, kiwango cha hewa mwilini, mapigo ya moyo na umeme wa moyo iwapo kutakuwa na shida taarifa itatumwa moja kwa moja kwa daktari kupitia simu yake ya mkononi ambayo itakuwa imeunganishwa na kifaa hicho”.“Baada ya daktari kupata taarifa tutatuma gari la wagonjwa ambalo litakuwa na daktari bingwa wa moyo pamoja na muuguzi ambao watakwenda kumuhudumia mgonjwa pia tutamuelekeza ndugu wa mgonjwa nini afanye wakati wataalamu wetu wanakwenda kutoa huduma kwa mgonjwa”, alisema Dkt. Kisenge.Dkt.Kisenge alisema huduma hiyo pia itawasaidia wagonjwa ambao wamekaa hospitali muda mrefu na wanataka kukaa karibu na ndugu zao nyumbani na wagonjwa ambao ni watu wazima sana ambao watahitaji kutibiwa wakiwa nyumbani.“Upatikanaji wa huduma hizi za matibabu ya kisasa ni jitihada za Mhe. Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuboresha huduma za afya nchini, hivi sasa katika Taasisi yetu tuna magari ya wagonjwa sita ambayo yanatusaidia kutoa huduma kwa wagonjwa”, alisema Dkt. Kisenge.Akizungumza kuhusu huduma nyingine zitakazotolewa kwa wagonjwa walioko majumbani daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Smitha Bhalia alisema ni pamoja na wagonjwa waliopata kiharusi ambao watapata huduma ya mazoezi ya viungo na wenye shida ya lishe watapewa ushauri na kuelekezwa vyakula gani watumie.Dkt. Smitha alisema wagonjwa wengine ambao watapata huduma ya kufuatwa nyumbani ni wale ambao amefanyiwa upasuaji wa moyo na wanahitaji kusafishwa kidonda wauguzi watawafuata na kuwapa huduma hiyo pia kuna wagonjwa ambao wanahitaji kukaa na muuguzi wa kumuhudumia kwa saa 24 nao pia watapata huduma hiyo.“Huduma hizi zitatolewa kwa wagonjwa ambao wamepimwa na kuonekana kuwa wanaweza kupata huduma wakiwa nyumbani na kwa ambao hali yao haiwaruhusu kutibiwa wakiwa nyumbani watapelekwa JKCI kwaajili ya matibabu”.“Kuna huduma ya gari la wagonjwa ambapo mgonjwa akizidiwa atapiga simu namba 0688027982 na 0788308999 nasi tutamfuata na kwenda kumuhudumia, tutaangalia maendeleo ya afya yake na kuona kama tumlete hospitali au abaki nyumbani na kuendelea na dawa”, alisema Dkt. Smitha.
Published 2024-04-23 07:40:32 by JKCI
Watoto 60 wenye matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo ambayo ni matundu na mishipa ya damu kutokukaa katika mpangilio wake wanatarajia kufanyiwa upasuaji wa moyo katika kambi maalumu ya matibabu inayofanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).Kambi hiyo ya upasuaji mkubwa na mdogo wa moyo ya siku nane inafanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka mradi wa Little Heart wa Shirika la Muntada Aid lenye makao yake makuu mjini London nchini Uingereza.Akizungumza leo jijini Dar es Salaam kuhusu kambi hiyo Mkuu wa Kitengo cha Magonjwa ya Moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt.Sulende Kubhoja alisema katika kambi hiyo watoto wanafanyiwa uchunguzi, ambao wanakutwa na matatizo yanayohitaji kufanyiwa upasuaji wanafanyiwa upasuaji mdogo wa moyo kwa njia ya tundu dogo kupitia mtambo wa Cathlab pamoja na upasuaji mkubwa wa moyo wa kufungua kifua. “Tunawaomba wazazi wenye watoto wanaosumbuliwa na matatizo ya moyo yakiwemo matundu, mishipa ya damu na valvu za moyo (PDA, ASD, VSD for device closure na PS) wawalete katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwaajili ya kufanyiwa uchunguzi na kupata matibabu”.“Pia tunawaomba madaktari kutoka Hospitali zote nchini kuwapa rufaa watoto wenye matatizo hayo ili waje JKCI kwaajili ya kupata huduma za matibabu”, alisema Dkt. Kubhoja ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto.Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Upasuaji Dkt. Angela Muhozya, Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa JKCI Alex Joseph alisema wanatarajia kufanya upasuaji mkubwa wa kufungua kifua kwa watoto 20 .“Mgonjwa anayefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo anahitaji damu nyingi, tunashukuru tuna damu ya kutosha kwaajli ya watoto wanaofanyiwa upasuaji, tunawaomba wananchi muendelee kuchangia damu kwaajili ya watoto wetu wanaofanyiwa upasuaji wa moyo”, alisema Dkt. Alex.Kwa upande wake daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Stella Mongela alisema katika kambi hiyo watoto 40 watafanyiwa upasuaji mdogo wa moyo kwa njia ya tundu dogo kupitia mtambo wa Cathlab.“Katika upasuaji huu mdogo wa moyo tunatumia mtambo wa Cathlab ambao ni maabara maalumu inayotumia mionzi kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu ya moyo, matibabu tunayoyatoa ni ya kuziba matundu ya moyo pamoja na kuzibua mishipa ya damu ya moyo iliyoziba”, alisema Dkt. Stella.Naye Meneja wa miradi wa Shirika la Muntada Aid Kabir Miah alisema Shirika hilo lina miradi mingi ikiwemo ya afya, elimu na maji na linafanya kazi katika nchi mbalimbali duniani ambapo katika bara la Afrika linafanya kazi katika nchi 30 ikiwemo Tanzania.“Hii ni mara ya tisa tunakuja Tanzania kuwasaidia watoto wenye matatizo ya moyo na tumeshafanya upasuaji kwa watoto 475,tunafurahi kuona tumeweza kuokoa maisha ya watoto ambao baada ya kupona wameweza kuendelea na maisha yao kama watoto wengine ambao hawakuzaliwa na matatizo ya moyo”, alisema Kabir.
Published 2023-10-20 09:38:48 by JKCI Admin
Dear Researchers/ ScientistsJakaya Kikwete Cardiac Institute (JKCI), is hosting an international conference called Heart Team Africa – CARDIONTAN, from February 9th – 10th, 2024, at the Golden Tulip Hotel, Zanzibar. The conference focuses on advances in cardiovascular care, with eight subthemes including clinical cardiology, cardiothoracic surgery, diagnostic imaging, nursing, anesthesia, critical care, interventional cardiology, and cardiovascular disease prevention. With 300 delegates from over 40 countries, it aims to enhance cardiovascular care and save lives. Don’t miss out on presenting in this year’s scientific conference that will involve presentations of abstracts for both local and international delegates. You can submit abstract through email address: heartteamafrica@gmail.com Dead line for submission : 15th December, 2023Also register to attend the conference through Ms Zuhura Nassor at +255 716 623 181 zuhurakhamisnassor@gmail.com or Dr. Khuzeima Khanbhai at +255 787 460 653 drkhuz@gmail.com who will generate codes and give you control numbers for payment of the fee.
Published 2023-10-20 09:39:38 by JKCI Admin
Dear ParticipantsJakaya Kikwete Cardiac Institute (JKCI), East Africa's largest Cardiac Centre, is hosting an international conference called Heart Team Africa – CARDIONTAN, where by presentations of abstracts for both local and international delegates will be done on the 09th and 10th February 2024 at the Golden Tulip Hotel, Zanzibar. In order to enhance cardiovascular care, we have organized a workshop (pre - conference activities) on the 8th February 2024 for hands-on training that will be held at Verde Hotel, Zanzibar. With 300 delegates from over 40 countries to share scientific experiences, that will enhance the provision of cardiovascular care and build capacity for the heart team so as to save lives. It is in this regard, that your participation in the conference will be highly valued in achieving this objective. To register, send full names and designations to Ms. Zuhura Nassor at +255 716 623 181 email address: zuhurakhamisnassor@gmail.com or Dr. Khuzeima Khanbhai at +255 787 460 653 email address: drkhuz@gmail.com, who will generate codes and provide control numbers for fee payment.
Published 2023-10-18 09:03:37 by JKCI Admin
CHINA, Beijing: The Chinese government said on Thursday it would push for more financial support to the Jakaya Kikwete Cardiac Institute (JKCI) partly to transform the latter into the top cardiac centre in the continent.China International Development Cooperation Agency (CIDCA) Chairman, Mr. Luo Zhohui told Tanzania’s Finance Minister Dr. Mwigulu Nchemba in Beijing the new support will cover construction of modern buildings, installation of modern medical equipment and training.The two had met briefly during Dr. Mwigulu’s official working visit in China. The two vowed to continue promoting cooperation between the two countries.